Kampasi ya Singida

Kampasi ya Singida ni miongoni mwa Kampasi sita za Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania.  Kampasi ya Singida   ilianzishwa rasmi Mwezi wa Saba (7) mwaka 2011 ikiwa ni kampasi ya nne kuanzishwa kati ya Kampasi sita za Chuo.  Kuanzishwa kwa Kampasi ya Singida ni utekelezaji wa maelekezo aliyoyatoa aliyekuwa Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda tarehe 23 Novemba, 2009 wakati akifungua kampasi ya Mtwara. Kamapasi ya Singida ipo Barabara ya Uwanja wa Ndege, Kata ya Mandewa -Manispaa ya Singida.



Kampasi ya Singida ipo Barabara ya Uwanja wa Ndege, Kata ya Mandewa -Manispaa ya Singida. Kampasi ya Singida inatoa kozi mbalimbali kuanzia ngazi ya astashahada na stashahada. Miongoni mwa kozi hizo ni pamoja na astashahada ya utunzaji wa kumbukumbu, astashahada ya uhazili, astashahada ya menejimenti ya rasilimaliwatu na astashahada ya utawala wa umma (NTA,4) pamoja na  stashahada ya utunzaji wa kumbukumbu, stashahada ya uhazili, stashahada ya menejimenti ya rasilimaliwatu na stashahada ya utawala wa umma (NTA 5& 6). Aidha, Kampasi ya Singida ni kituo cha mafunzo ya muda mfupi kwa watumishi wa umma, shauri za kitaalamu na ni kituo  cha  mafunzo na mitihani kwa watumishi wa umma

Ili kuwasaidia wanachuo kupata ujuzi kwa lengo la kukuza weledi wao na maendeleo ya taaluma  zao  katika fani mbalimbali walizochagua , kampasi ya Singida ipo katika mazingira mazuri ambayo yana-:

  1. Huduma za  uhakika za  kifedha na chakula zinazotolewa na taasisi mbalimbali za kifedha na chakula ili  kusaidia upatikanaji rahisi wa huduma za fedha na chakula kwa gharama nafuu
  2. Hali ya hewa nzuri  inayofungamanishwa  na mazingira mazuri ya kujisomea  na kujifunza
  3. Huduma nzuri za hosteli na malazi zinazopatikana kwa bei rahisi. Kampasi inatoa huduma za hosteli zinazopatikana ndani na nje ya chuo. Hosteli za nje ya kampasi zinapatikana kwa kushirikiana na wamiliki binafsi lakini chini ya usimamizi wa menejimenti ya Kampasi.  Ghrama za hostei kwa muhula ni kati ya Tsh. 150,000-200,000 kutegemeana na ubora  wa hosteli husika
  4. Huduma nzuri za  afya ambazo hutolewa kupitia vituo vya kutolea huduma za afya vinavyomilikiwa na serikali na taasisi binafsi  hususan Hospitali ya Manispaa ya Singida, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa , Kituo cha afya cha Tumaini, Kituo cha Afya MICO n,k. Vituo vyote hivi vya kutolea huduma za afya vinafikika kirahisi, vinatoa huduma bora  na vipo karibu na chuo.
  5. Huduma za kuabudu kwa dini zote na madhehebu yote. Kampasi ya Singida ipo karibu kabisa na nyumba mbalimbali za kuabudia (makanisa na misikiti) kwa wanachuo wa dini zote. Aidha, Kampasi ya Singida imeruhusu wanachuo kutumia ukumbi wa chuo kwa ajili ya kuabudia pale unapohitajika.
  6. Huduma za viwanja vya michezo mbalimbali ili kuwapa wanachuo pamoja na walimu wao  fursa ya kushiriki kwenye michezo mbalimbali ili kuimarisha afya zao  na kuboresha maendeleo ya taaluma zao. Baadhi ya viwanja vya  michezo vilivyopo ni pamoja na viwanja vya mpira wa miguu, mpira wa pete  na mpira wa wavu
  7. Huduma za bima za  afya ambazo zinatolewa kwa ushirikiano na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) ili kurahisisha upatikanaji wa afya bora na kwa wakati kwa wanachuo.
  8. Huduma za ushauri  hususan ushauri kuhusu mambo ya kiafya,  kitaaluma, kiuchumi na kifedha, na kisaikolojia  hutolewa kwa wanachuo wenye uhitaji na wanachuo wote kwa ujumla
  9. Huduma nzuri za ulinzi na usalama wakati wote hivyo kuwasaidia wanachuo kujifunza pasipo hofu zozote za kiusalama.

Kampasi ya Singida inatoa huduma zake za kitaaluma kupitia kwenye madarasa ya kisasa na yanayopitisha hewa ya kutosha, maabara za kisasa za kuchapia, maabara za kisasa za komputa, maktaba nzuri yenye vitabu vya kisasa, mtandao wa kutosha kuwezesha wanachuo kujitafutia mahitaji yao ya kujifunzia kwenye vyanzo mbalimbali, n.k. Aidha, Kampasi ina watumishi ( Walimu na Wasiowalimu) wanaojituma, wenye weledi, hamasa na wenye vipaji vya kutosha kufanya kazi ya kuwajengea uwezo wanachuo katika Nyanja tofauti tofauti kwa utiifu na uaminifu mkubwa.  

Mkurugenzi wa Kampasi

Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania

S.L.P 1534

Singida

Simu: +255 26 2502933/3082

Nukushi +255 26 250 3082

Barua Pepe: singida@tpsc.go.tz

 

Feedbacks

Mrejesho, Malalamiko au Wazo