Mitihani ya Utumishi wa Umma kwa watumishi wa umma ilianzishwa kwa mujibu wa kifungu cha (I) cha Kanuni za Kudumu za Utumishi wa Umma. Pia Sheria ya Utumishi wa Umma namba 8 ya mwaka 2002 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2008 ilitoa mamlaka kwa Chuo cha Utumishi wa Umma kuendesha hiyo tangu mwaka 2003.
Mitihani ya utumishi wa Umma hufanyika mara mbili kwa mwaka (Februari na Agosti) kwa muda wa wiki nne. Wiki tatu za kwanza ni za darasa la mapitio (review classes) na wiki moja ya mwisho ni kwa ajili ya watumishi kufanya mitihani yenyewe.
Kada zinazohusika na mitihani ya utumishi wa umma na programu za mapitio ni pamoja na:
- Usimamizi wa Nyaraka kwa Wasaidizi wa Kumbukumbu (Higher Standard Records Management)
- Mtihani wa Waendeshaji Simu (Telephone Operators);
- Maendeleo ya Usimamizi kwa Wasaidizi wa Watendaji Wakuu I;
- Maendeleo ya Usimamizi kwa Wasaidizi wa Watendaji Wakuu II;
- Mtihani wa Umahiri kwa Maafisa Rasilimali Watu;
- Mtihani wa Umahiri kwa Maafisa Kumbukumbu;
- Mtihani wa Umahiri kwa Maafisa Ustawi wa Jamii
- Mtihani wa Umahiri kwa Maafisa Kazi;
- Sheria kwa Maafisa Tawala;
- Sheria kwa Maafisa Watendaji wa Kata/Tarafa; na
- Mtihani wa umahiri kwa Maafisa Maendeleo ya vijana;
MITIHANI YA WATUMISHI WA UMMA - MACHI, 2026
Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC), kinawatangazia watumishi wote wa Umma wanaotarajia kufanya mitihani ya Utumishi wa Umma kwa mwezi Machi, 2026 kuwa kozi ya mapitio ya mitihani itafanyika kuanzia tarehe 30 machi hadi 17 Aprili, 2026 kwa watahiniwa watakaohudhuria kwa njia ya ana kwa ana na kwa upande wa mapitio kwa njia ya mtandao yataanza tarehe 3 Machi hadi 10 Aprili, 2026 na kufuatiwa na mitihani itakayofanyika kuanzia tarehe 20 hadi 24 Aprili, 2026 katika vituo vyote vya Dar es Salaam, Tabora, Mtwara, Singida, Tanga, Mbeya na Dodoma.
BONYEZA HAPA KUJISAJILI - MAFUNZO KWA NJIA YA MTANDAO (ONLINE REVIEW CLASSES)
BONYEZA HAPA KUPAKUA FOMU YA MAOMBI ( ANA KWA ANA)

