Imewekwa: 11 Nov, 2025

Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania anapenda kuwatangazia wahitimu wote na wadau wa Chuo kuwa, Mahafali ya arobaini na Mbili (42) ya Chuo cha Utumishi wa Umma kwa Kampasi zote yanatarajiwa kufanyika   siku ya Ijumaa, tarehe 28  Novemba, 2025 katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere(JNICC), Dar es Salaam  kuanzia saa tatu (03.00) Asubuhi.

Aidha, wahitimu wote wanahimizwa kuhudhuria mazoezi (Rehearsal) yatakayofanyika siku ya Alhamisi tarehe 27 Novemba 2025 katika Kampasi ya Dar es Salaam  kuanzia saa nane (08.00) mchana. Wahitimu wanatakiwa kuvaa Joho na  suti ya rangi nyeusi au dark blue. 

Wahitimu wanatakiwa kuthibitisha ushiriki wao kupitia namba. 0679031848/0629820870.

ORODHA  YA WAHITIMU

KAMPASI YA DAR ES SALAAM

KAMPASI YA TABORA

KAMPASI YA MTWARA

KAMPASI YA MBEYA

KAMPASI YA TANGA

KAMPASI YA SINGIDA

 

Limetolewa na

Kitengo cha Mawasiliano na Masoko

Feedbacks

Mrejesho, Malalamiko au Wazo